Baada ya ushindi wa kwanza ulioambana na vituko, Sunderland chini
Roberto Di Canio leo timu hiyo imeonyesha haikubahatisha.
Maana imeichapa timu ngumu ya Everton kwa bao 1-0 na kufanya mashabiki
wake wachanganyikiwe kwa furaha.
Wakati mashabiki walikuwa na furaha kubwa, Di Canio raia wa Italia
alijikaza kisabuni na kuacha kushangilia kwa kuteleza kama alivyofanya katika
mechi iliyopita.
Safari hii aliendelea kushangilia kawaida na mashabiki wake walionyesha
bango linaloonyesha kwamba hawana na shida na Jose Mourinho kwa kuwa tayari
wana Di Canio.
Kocha huyo alipata wakati mgumu baada ya kutua Sunderland kutokana na
kushambuliwa sana na vyombo vya habari kwamba wakati akicheza West Ham alikuwa
na hisia za Kifashisti.
0 COMMENTS:
Post a Comment