ANGETILE |
Aliyekuwa Katibu Mkuu wa TFF, Angetile
Osiah amekataa kulizungumzia suala la kuachishwa kwake kazi.
Hata hivyo akasema atafanya mkutano na
waandishi wa habari ndani ya siku mbili.
“Kwa sasa siwezi kuzungumza lolote,
lakini nitakutana na waandishi ndani ya siku mbili, hivyo kuweni na subira,”
alisema.
Osiah ameachishwa kazi huku mkataba wake
na TFF ukiwa umebaki miezi miwili.
Hata hivyo, Rais mpya wa TFF, Jamal
Malinzi amesema Osiah ataendelea kulipwa mshahara wake kwa miezi yote miwili.
Nafasi yake sasa ataikaimu, Boniface
Wambura ambaye ni msemaji wa shirikisho hilo.
Tayari Wambura ameishakabidhiwa kazi
hiyo iliyoachwa na Osiah ambaye ni mwandishi mwenzake wa habari.
0 COMMENTS:
Post a Comment