Timu ya
Coastal Union U 20 imkefanikiwa kutwaa ubingwa wa Kombe la Uhai kwa kuichapa
Yanga kwa mabao 2-0.
Coastal
Union ambayo iliingia fainali baada ya kuivua ubingwa Azam Fc ilionyesha soka
safi na la kuvutia. Na Juma Mahadh na Ally Ufud wakafanya kweli kwa kufunga mabao hayo mawili.
Baada ya
kupata bao la kwanza, Coastal ilizidi kuwa bora na kuipa Yanga wakati mgumu
zaidi.
Bao la pili
lilipatikana katika dakika ya 88 huku Yanga wakiamini walikuwa wanakaribia
kusawazisha.
0 COMMENTS:
Post a Comment