Kocha mpya wa
Simba, Zdravko Logarusic amewasili nchini leo na kusema yuko tayari kwa ajili
ya kuanza kazi.
Awali
ilielezwa kocha huyo hatakuja nchini kwa kuwa Mwenyekiti wa Simba
aliyesimamishwa, Ismail Aden Rage alitangaza kuwarudisha Abdallah Kibadeni na Jamhuri Kiwhelo 'Julio'. Lakini wapi bana, kocha huyo ametua Dar tayari kwa kuanza kazi.
Kocha huyo
ameonyesha kweli yuko shap maana ameishakagua kiwanja cha Kinesi na mara moja
ameingia katika mitaa ya Dar.
“Niko
tayari kwa kazi, nataka kufanya vizuri lakini najua kuwa maandalizi ndiyo kitu
muhimu.
“Lakini
siwezi kusema sana kwa sasa hadi nitakapowaona wachezaji,” alisema Logarusic.
Wajumbe wa kamati ya utendaji ya Simba walijitokeza uwanjani wa ndege kumpokea wakiongozwa na Swed Nkwabi ambaye ni kaimu makamu mwenyekiti.
Wengine waliokuwepo ni Danny Manembe na Said Pamba ambao waliondoka na kocha huyo uwanjani hapo.
0 COMMENTS:
Post a Comment