MUSOTI (KUSHOTI) WAKATI AKIITUMIKIA SIMBA. HAPA AKIWA MAZOEZINI NA SHABANI KISIGA KAMBINI ZANZIBAR. |
Beki wa zamani
wa Simba, Donald Musoti, ameendelea kuibana klabu hiyo katika kesi ya madai
yake ya kuvunja mkataba kwa kusema kuwa Simba imeshindwa kuwasilisha vielelezo
vya ushahidi katika Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa).
Akizungumza kutoka Nairobi, Kenya, Musoti alisema Fifa wameamua kesi yake
isikilizwe kuanzia wiki ijayo kwa upande mmoja kutokana na Simba kushindwa
kuwasilisha vielelezo vyao kama walivyotakiwa.
“Mwanasheria
wangu, Felix Majani, ameniambia kesi itasikilizwa kwa upande mmoja baada ya
Simba kushindwa kuwasilisha vielelezo vyao kama walivyoombwa awali.
“Nadhani
watakuwa wamekosa cha kupeleka kwa sababu hakuna kitu ambacho kinaweza
kuwasaidia kujitoa katika kesi hii.
“Unajua
sikutaka kesi yangu isikilizwe na TFF kwa sababu ni wazi nisingeweza kushinda
kutokana na wao wangefanya ujanja-ujanja mwingi lakini Fifa hakuna kitu kama
hicho, lazima haki yangu ipatikane,” alisema Musoti.
Simba ilivunja
mkataba na beki huyo na nafasi yake kuchukuliwa na Emmanuel Okwi, kesi hiyo
ilisimamishwa kusikilizwa baada ya Simba kuomba kupewa muda mpaka Oktoba 23,
mwaka huu kuwasilisha vielelezo vyao vya kuvunjwa kwa mkataba huo.
0 COMMENTS:
Post a Comment