March 18, 2015


Kiungo mkabaji tegemeo wa Simba SC, Jonas Mkude, ameshangazwa na kitendo cha kutoitwa kwenye kikosi cha timu ya taifa, Taifa Stars kilichoitwa hivi karibuni kwa ajili ya mchezo wa kirafiki dhidi ya Malawi.

Mchezo huo unatarajiwa kupigwa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza, Machi 29, wakati timu ikitazamiwa kuingia kambini Machi 22, mwaka huu.

Mkude ambaye amekuwa aking’ara kwenye mechi kadhaa za Simba, amesema hajui kwa nini hajaitwa kwenye kikosi cha timu hiyo ingawa bado anashangazwa na hali hiyo akiamini kuwa huu ndiyo muda muafaka kwake kulitumikia taifa kutokana na mchango anautoa kwa klabu yake.

“Sijajua kwa nini sijaitwa, japokuwa naamini huu ndiyo muda wangu muafaka sasa wa kutumika Stars lakini siwezi kujua mwalimu anawaza nini kwa kuwa yeye ndiyo mtu wa mwisho kwenye kila kitu, ila pia nashangaa kuna wachezaji wameitwa na kwenye klabu zao hawatumiki ipasavyo, labda kocha anaweza kuwa na mipango ya ziada, cha msingi niitakie timu kila la kheri tushinde huo mchezo ambao ni muhimu pia kwetu,” alisema Mkude.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic