![]() |
| CHINI (WA TANO KUSHOTO) AKIWA NA KIKOSI CHA STAND UNITED. |
Mnigeria
wa Stand, Abasarim Chidiebele amesema atapambana kumfikia mshambuliaji Didier Kavumbagu wa Azam FC kwa
mabao na ikiwezekana ampite.
Chidi anataka kumvuka Kavumbagu raia wa Burundi ambaye ana mabao 10 sasa katika Ligi Kuu Bara.
Chidiebele aliyewahi kufanya majaribio
Simba na kuachwa, sasa ana mabao saba, hivyo anashika nafasi ya tatu kwa
ufungaji nyuma ya Rashid Mandawa wa Kagera Sugar mwenye mabao nane na kinara
Kavumbagu mwenye mabao kumi.
Kavumbagu alifikisha bao lake la kumi juzi
Jumatatu alipofunga bao pekee dhidi ya Ndanda FC kwenye Uwanja wa Azam Complex.
Saa chache baada ya kufunga bao hilo,
Chidiebele akasema: “Najua Kavumbagu kafikisha mabao kumi lakini nitahakikisha
napambana na kufunga katika kila mechi ili nimfikie na kumpita.”
Alisema anajua Kavumbagu anasaidiwa sana na
wachezaji wenzake kufunga jambo ambalo hata katika timu yake lipo, hivyo
amepanga kufunga katika kila mechi iliyo mbele yao ili aongoze kwa ufungaji.
Mechi nyingine za Stand ni dhidi ya Mtibwa
Sugar, Polisi Moro, JKT Ruvu, Azam, Coastal Union na Ruvu Shooting.








0 COMMENTS:
Post a Comment