Mashabiki wa Yanga na wale wa Azam FC, jana walianzisha
uhusiano wa muda walipokutana pamoja na kushangilia kwa pamoja.
Mfano mzuri ni mashabiki maarufu wa timu hizo, Ally Yanga na
Steve Kulialia waliposhangilia kwa pamoja wakati Yanga ikifungwa kwa mabao 2-1
na Azam FC kupata nafasi ya kushiriki michuano ya kimataifa kwa kuwa
imejihakikishia nafasi ya pili.
Mashabiki wengine wa Yanga na wale wa Azam FC walikuwa
wakizunguka kila sehemu pamoja wakishangilia mechi hiyo iliyoonekana kama ya
kirafiki vile.
Hata baada ya mechi hiyo, viongozi na wachezaji wa Azam FC
waliungana pamoja na kushangilia.
0 COMMENTS:
Post a Comment