October 7, 2015


Yaleyale! Jinamizi la timu ya Kagera Sugar kukimbia makazi limeendelea kuwatesa, baada ya kutangaza kuachana na Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, ambao wamekuwa wakiutumia kama uwanja wao wa nyumbani.


Timu hiyo ambayo inakodi uwanja kutokana na wao wa Kaitaba kuwa kwenye ukarabati wa kisasa, imesema kwa sasa mikakati iliyopo ni kutaka kusogea karibu na Ukanda wa Pwani ambako ndiko kuna timu nyingi za ligi kuu.

Ikumbukwe kuwa msimu uliopita Kagera walitumia viwanja viwili tofauti; CCM Kirumba wa Mwanza, kabla ya kuhamishia makazi Kambarage, Shinyanga, kwa kile kilichosemwa kuwa Kirumba walikuwa wakifanyiwa hujuma za kishirikina kutoka kwa wanachama waliodhaniwa kuwa wa Toto Africans.

Mratibu wa timu hiyo, Mohamed Hussein ameliambia Championi Jumatano kuwa; “Tunataka kusogea karibu na Ukanda wa Pwani maana timu nyingi ziko huko. Lakini pia hata ratiba ya ligi kuu inatubana sana, tofauti na misimu iliyopita mechi zilikuwa wikiendi tu.

“Lakini msimu huu tunacheza mara mbili kwa wiki na huku ni mbali sana- wachezaji hawapati muda wa kupumzika, hivyo tumeona tusogee karibu na sehemu yenye timu nyingi,” alisema.


Hata hivyo, imeaminika kuwa matokeo mabovu kwenye uwanja huo pia yamechangia Wakata Miwa hao kukimbia.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic