TEGETE (KULIA) AKIWA KATIKA MAZOEZI YA MWADUI FC |
Kocha Mkuu
wa Mwadui FC, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ amesisitiza kwamba mshambuliaji Jerry
Tegete anaweza kurejea katika kikosi cha timu ya taifa, Taifa Stars.
Julio
amesema Tanzania bado ina tatizo la wafungaji na Tegete ambaye ameanza
kuonyesha cheche zake kwa kufunga bao katika mechi yao iliyopita ana nafasi ya
kurejea Stars kama atajituma zaidi.
“Kama
atajituma zaidi mazoezi na katika mechi, basi ana nafasi ya kurejea Taifa
Stars,” alisema.
0 COMMENTS:
Post a Comment