February 12, 2017


Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger amewashukuru waandishi wa habari kwa kumtaka apumzike lakini amewaambia wazi, “wasahau”.

Wenger amesema hana mpango wa kuachia ngazi licha ya kuwepo kwa taarifa Arsenal ingependa kumchukua Diego Simeone kutoka Atletico Madrid ya Hispania kuchukua nafasi yake.

Mara baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Hull City yeye akiwa jukwaani, Wenger amesema, hana mpango wa kupumzika.

“Nashukuru sana kwa nia yenu njema ya kunitaka kupumzika. Lakini sihitaji kufanya hivyo kwa sasa,” alisema Wenger.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic