March 14, 2018


Na George Mganga

Kocha Msaidizi wa Stand United, Athuma Bilal 'Bilo', ametoa mtazamo wake kuhusiana na mwenendo wa Shirikisho la Soka nchini namna unavyoenda tangu uingie madarakani Agosti 2017.

Bilo ameeleza kuwa TFF ya sasa iliyo chini ya Rais Wallace Karia, imejitahidi kufanya marekebisho kadhaa ambayo hayakuwa yanaonekana kipindi cha uongozi uliopita.

Kocha amesema wakati wa uongozi uliopita ilikuwa ni ngumu kwa timu nyingi kwenye ligi kupata matokeo au pointi tatu halali kama ambavyo imekuwa hivi sasa.

Bilo ambaye kikosi cha Stand United kipo katika nafasi ya 11 kwenye msimamo wa ligi, ametoa sifa pia kwa waamuzi walio chini ya watala wa awamu hii kuwa wamekuwa wakijitahidi ukiachana na kipindi cha nyuma.

Licha ya hayo, Bilo ameliomba Shirikisho kuendelea kuboresha mabadiliko haswa kwa waamuzi ambao wengi wamekuwa wakiharibu taswira ya timu kupata matokeo halali, pia kudhorotesha mpira wa Tanzania.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic