September 25, 2018


Baada ya Simba kushinda jioni, Yanga ilijibu mapigo kwa kushinda usiku huku Amissi Tambwe akirejea kwenye makali yake kwa ku­funga mabao mawili ‘brace’.

Timu hizo zimeshinda kuelekea kwenye mchezo wao utakaochezwa Septemba 30, na sasa kila upande baada ya ushindi huo ni kama wanasema: “Waleteni sasa” kutokana na kuji­amini kwamba unaweza kuibuka na ushindi.

Yanga juzi iliichapa Sin­gida United mabao 2-0 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Sa­laam, huku Ibrahim Ajibu akipiga pasi ya bao la kwanza la Tambwe na kufikisha jumla ya asisti tano katika mechi nne ambazo Yanga imecheza kwenye Ligi Kuu Bara.

Ajibu alitoa asisti (pasi za mabao) tatu katika mechi dhidi ya Stand, akatoa asisti nyingine dhidi ya Coastal, kabla ya jana kutoa nyingine.

Ushindi huu unaashiria sasa Yanga ipo tayari kukutana na Simba Jumapili ijayo, ikiwa imeshinda mechi zote nne ilizocheza kwenye Ligi Kuu Bara na kupanda kileleni mwa msimamo.

Tambwe ambaye wengi walianza kumuona amechuja na ‘ameshazeeka’, alianza kufunga dakika ya 29 kwa kichwa akiunganisha krosi ya Ajibu, aliongeza bao la pili dakika ya 45+2 kwa pasi fupi ya Gadiel Michael na kuamsha shangwe la mashabiki wa timu yake.

Kocha Mwinyi Zahera alifanya maamuzi magumu kwa kuamua kutowatumia beki Kelvin Yondani na washambuliaji wake hatari Heri­tier Makambo na Mrisho Ngassa, na akawashangaza wengi alipoamua kuwaanzisha Tambwe na Matheo Anthony.

Aliamua kuwapumzisha nyota hao kwa kile kilichoonekana ni mchezo dhidi ya watani Jumapili hii.

Yanga: Benno Kakolanya, Paul God­frey, Gadiel Michael, Abdallah Shaibu, Andrew Vincent ‘Dante’, Feisal Abdal­lah, Deus Kaseke, Papy Tshishimbi, Tambwe, Ajibu na Anthony.

Singida: David Kissu, Kennedy Juma, Mohammed Tello, Elisha Muroiwa, Rajab Zahir, Yusuph Kagoma, Athanas Mdamu, Amara Diaby, Hans Kwofie, Kenny Ally na Geofrey Mwashiuya.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic