MANARA AAMUA KUWACHANA BAADHI KUHUSU KAPOMBE, AJISHTUKIA NA KUOMBA RADHI TFF KIAINA
Ofisa Habari wa klabu ya Simba ameibuka na kueleza namna ambavyo hajaeleweka kuhusiana na andika lake fupi la jana juu ya beki wa Simba, Shomari Kapombe.
Manara ameandika kuwa hakumaanisha TFF huwa hawahusiki kuwasaidia wachezaji pale wanapoumia katika timu ya taifa bali wao kama klabu wameamua kumuwahisha Kapombe kwa ajili ya matibabu.
"Niwasihi watu wetu tunaposoma vitu makini tusizushe hisia zetu . Jana niliandika kuhusu Beki wa nchi Shomari Kapombe kwenda kutibiwa nje na nikaeleza kwa kina! Kuna wasiotaka kuelewa eti TFF hawahudumii wachezaji.
"Narudia TFF na Simba siku zote kama inavyopaswa tupo pamoja, na katika hili mnielewe hivyo.
"Na naomba msamaha kwa TFF kwa kutoeleweka vema!
Sasa tayari Shomari ashaanza vipimo na tutawajuza zaidi" ameandika Manara.
0 COMMENTS:
Post a Comment