December 19, 2020

 


BAADA ya kusaini dili la mwaka mmoja kiungo fundi wa kuchezea mpira, Haruna Niyonzima amesema kuwa anaamini timu hiyo itatwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara. 


Yanga ipo nafasi ya kwanza ikiwa na pointi 37 baada ya kucheza jumla ya mechi 15.


Imeshinda mechi 11, sare nne na haijapoteza mchezo, ikiwa imefunga mabao 22, Niyonzima amefunga bao ilikuwa ni Uwanja wa Mkapa wakati Yanga ikishinda mabao 3-0.


Niyonzima ameongeza mkataba wa mwaka mmoja ndani ya Yanga hivyo ataendelea kupambana mbele ya Kocha Mkuu,  Cedric Kaze. 


Nyota huyo amesema:"Nipo Yanga kwa sasa na ninafuraha kubwa, imani yangu ni kuona kwamba tunatimiza malengo tuliyojiwekea ili kufikia malengo tuliyojiwekea.


"Tunahitaji ubingwa na hilo lipo wazi, tunaamini kwamba tutafikia malengo hayo," .

3 COMMENTS:

  1. HAKUNA NOMA WE PAMBANA TU MZAZI, ILA SIO RAHISI KAMA UNAVYODHANI SHINDENI MECHI ZENU ZOTE TU

    ReplyDelete
  2. Kwa maana hii ni mala yake ya kwanza kubeba Ubingwa akiwa Yanga?

    ReplyDelete
  3. hata alivyorudi kucheza Tanzania baada ya kutemwa na Simba alikuw a akisema hivyo

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic