July 25, 2014

MWANA FA


Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi, mapema wiki hii alijikuta akijibizana hoja na mwanamuziki wa Bongo Fleva, Hamis Mwinjuma ‘Mwana FA’ juu ya mwelekeo wa timu ya taifa, Taifa Stars, mara baada ya matokeo ya mabao 2-2 dhidi ya Msumbiji kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar, Jumapili iliyopita.


Mwana FA ambaye ni mdau mkubwa wa soka, alitoa hoja kwa Malinzi katika mtandao wa Twitter, ambapo alilalamika juu ya mahudhurio hafifu ya mashabiki katika mechi, ambapo ilielezwa yalitokana na ukubwa wa kiingilio kilichopangwa na TFF, lakini Malinzi alipinga hoja hiyo.
 
MALINZI
Sehemu ya majibizano yao ilikuwa hivi:
Mwana FA: Mheshimiwa Jamal Malinzi, nadhani hii kauli inatufaa na sisi...mahudhurio hafifu yanashusha morali za wachezaji wetu.

Malinzi: Mwana FA timu yoyote isiposhinda visingizio huwa havikosekani, Tanzania vs Zimbabwe waliingia watu 8,000 tu na tukashinda, juzi waliingia 20,000 tukapata sare.

Mwana FA: Jamal Malinzi siyo lazima kushinda kila siku, kama mwanamichezo naelewa, ni kuhusu kutengeneza mazingira 'yanayowabeba' wapenzi na wachezaji wetu.

Baada ya hapo, Malinzi hakutaka tena kuendelea na mjadala huo licha ya wadau wengine kuendelea kutoa maoni mtandaoni hapo, ambapo wengi wao walionekana kuitupia lawama TFF kutokana na kuweka kiingilio cha chini kuwa shilingi 7,000 ambacho walikilalamikia kuwa ni kikubwa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic