Mshambuliaji wa Barcelona, Neymar ameonyesha namna wa vijana wa Kibrazili wanavyowajali wapenzi baada ya kutuma ndege ya kukodi imsafirishe mrembo kutoka Serbia hadi Barcelona.
Neymar raia wa Brazil ametuma ndege ya
kukodi ambayo imembeba mpenzi wake Soraja Vucelic, taarifa zimeelezwa na gazeti
la udaku la Serbia la Kurir.
Imeelezwa, wawili hao walikutana kipindi cha
majira ya joto katika eneo la Ibiza wakati Neymar aliyekuwa amjeruhi
akipumzika.
Baada ya hapo, wawili hao walikubaliana
kukutana Oktoba na makubaliano ni Neymar kutuma usafiri.
0 COMMENTS:
Post a Comment