July 22, 2017



Everton imetoka sare ya bao 1-1 dhidi ya KRC Genk ya Ubelgiji katika mechi ya kirafiki kujiandaa na msimu mpya.

Mshambuliaji mpya wa Everton, Wayne Rooney amefunga bao lake la pili akiwa na Everton lakini Mtanzania Mbwana Samatta, naye amesema hapa, akamjibu.


Samatta aliifungia Genk bao la kusawazisha baada ya bao hilo la Rooney na mwisho kufanya timu hizo zimalize kwa sare hiyo ya 1-1.

Rooney alifunga bao lake katika dakika ya 45 na Everton iliyokuwa ugenini ikaenda mapumziko na bao hilo moja lakini Samatta akaisawazishia Genk katika dakika ya 55.


VIKOSI:
Genk: Jackers, Nastic, Brabec, Colley, Khammas, Berge, Malinovskyi, Trossard, Buffel, Benson, Samatta.
Subs: Coucke, Lenaerts, Wouters, Zhegrova, Naranjo, Vanzeir, Sabak, Schrijvers, Seigers, Heynen.
Goals: Samata 55


Everton: Pickford, Schneiderlin, Baines, Keane, Williams, Ramirez, Rooney, Gueye, Klaassen, Dowel, Holgate.
Subs: Joel, Stekelenburg, Lennon, Davies, Connolly, Calvert-Lewin, Mirallas, Kenny, McCarthy, Barry, Besic, Lookman, Martina.

Goals: Rooney 45 

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic