Ligi Daraja la Kwanza (FDL) kwa makundi yote matatu inaendelea
wikiendi hii ambapo kundi B litakuwa na mechi moja tu kati ya Lipuli na Mlale
JKT itakayochezwa kesho (Oktoba 12 mwaka huu) katika Uwanja wa Kumbukumbu ya
Samora mjini Iringa.
Transit Camp itakwaruzana na Tessema katika Uwanja wa Mabatini
mjini Mlandizi wakati Polisi Dar itaumana na African Lyon kwenye Uwanja wa
Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam katika mechi za kundi A zitakazochezwa
kesho (Oktoba 12 mwaka huu).
Mechi nyingine ya kundi hilo itachezwa keshokutwa (Oktoba 13 mwaka
huu) kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam kwa kuzikutanisha
Friends Rangers na Villa Squad.
Timu zote nane za kundi C zinashuka viwanjani kesho (Oktoba 12
mwaka huu) kusaka pointi tatu. Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma utakuwa mwenyeji
wa mechi kati ya Polisi Dodoma na JKT Kanembwa ya Kigoma.
Pamba na Mwadui zitacheza katika Uwanja wa CCM Kirumba jijini
Mwanza, Polisi Tabora itaikaribisha Toto Africans kwenye Uwanja wa Ali Hassan
Mwinyi mjini Tabora wakati uga wa Kumbukumbu ya Karume mjini Musoma utatumika
kwa mechi kati ya Polisi Mara na Stand United ya Shinyanga.
0 COMMENTS:
Post a Comment