October 11, 2013


BENCHI LA UFUNDI: KOCHA MKUU, Kibadeni, MSAIDIZI WAKE, Julio, MENEJA, Nico Nyagawa na KOCHA WA MAKIPA, James Kisaka.


Kiungo mkongwe wa Simba, Henry Joseph ataendelea kubaki timu katika timu ya pili, huo ni uamuzi wa benchi la ufundi la timu hiyo.

Kocha Msaidizi wa Simba, Jamhuri Kihwelo amesema Henry atabaki hapo hadi atakapobadilika.

“Anatakiwa kubadilika na kuonyesha juhudi, kwamba alikuwa anacheza nje basi atuonyesha kweli anastahili kuwa katika timu ya kwanza na atatoa msaada.

“Sisi hatujapenda vyimbo vya habari ambavyo vimeandika tofauti kama vile kufukuzwa Simba na vinginevyo, tulichofanya sisi ni kwa manufaa ya Simba.

“Kama Henry anagekuwa anajituma wala kusingekuwa na tatizo, tunajua alikuwa Ulaya na ndiyo maana tunategemea mchango mkubwa kutoka kwake. Tofauti tunaona si sahihi,” alisema Julio.

Henry alizuiwa kuendelea na mazoezi na Kocha Mkuu, Abdallah Kibadeni baada ya yeye kuanza kuomba apumzike.

Kibadeni alimueleza aendelee kupumzika baada ya kiungo huyo kurudi uwanjani na kutaka kuendelea na mazoezi.

Kabla ya hapo, Henry aliomba kupumzika kwa madai alikuwa amefanya mazoezi binafsi hivyo kuusikia mwili hauna nguvu.

Lakini ilielezwa alijichanganya kwani awali alimwambia Julio anajisikia ni mgonjwa halafu akamueleza Kibadeni kwamba alikuwa amechoka kutokana na mazoezi.

Kibadeni akamueleza akendelee kupumzika kwenye gari kama alivyokuwa amekaa hapo awali.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic