AMROUCHE |
Amrouche raia
wa Ubelgiji mwenye asili ya Algeria amesema mshambuliaji huyo wa Rwanda ana
uwezo mkubwa na kocha anatakiwa kuendelea kumuamini.
“Didier ni
kati ya washambuliaji bora katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati,” alisema
Amrouche ambaye aliwahi kumfundisha alipokuwa kocha wa timu ya taifa ya Burundi
kwa zaidi ya miaka mitatu.
“Ana uwezo wa
kuchezesha timu akiwa mbele, mzuri wa vichwa na wakati mwingine anakuwa mtulivu
sana katika umaliziaji.
“Nina imani
atafanya vizuri zaidi na hata kama asipofunga, anakuwa mtoaji mzuri wa pasi za
ufungaji kwa wenzake,” alisema.
Kavumbagu ni
kati ya washambuliaji tishio katika Ligi Kuu Bara ambayo inaendelea na tayari
Yanga imeshika usukani baada ya kuichapa JKT Ruvu mabao 4-0, jana.
0 COMMENTS:
Post a Comment