Mwenyekiti wa
Yanga, Yusuf Manji amesema hatakuwa na tatizo kama Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi
Kuu Bara, Yahaya Mohammed atataka kumtembelea ofisini kwake.
Manji amesema
kawaida waungwana husikiliza kwanza wanachoelezwa kabla ya kuzungumza.
“Nitamkaribisha
kama kweli atataka kunitembelea na kuzungumza na mimi. Sina tatizo katika hilo.
“Mazungumzo
ndiyo yatatoa majibu ya kila mmoja wetu anachokitaka au kukiamini ni bora kwake
na maendeleo ya mpira wa Tanzania,” alisema.
Hivi karibuni
mara baada ya Yahaya kuchukua nafasi ya uenyekiti, alisema atamtembelea Manji
ofisini kwake ili wazungumze kuhusiana na tofauti zilizojitokeza kati ya Yanga
na bodi hiyo.
Bodi hiyo
imeingia mkataba na Azam TV kuonyesha mechi za ligi kuu live, lakini Yanga
imekuwa ikitaka kulipwa zaidi na kutaka kutofautishwa na timu nyingine ndogo
ambazo hazina mashabiki wengine kama ilivyo yenyewe.
0 COMMENTS:
Post a Comment