November 2, 2013


Rais aliyepita wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Leodeger Tenga amekabidhi fedha na mali ya jumla ya Sh bilioni 1.3 kwa rais mpya.


Rais Mpya wa TFF, Jamal Malinzi amekabidhiwa vitu hivyo leo katika ofisi za shirikisho hilo Karume, Ilala jijini Dar es Salaam.
Katika vitu hivyo ni pamoja na eneo la Krume lenye ukubwa wa ekari 8.2 ndani yake kukiwa na uwanja wa Karume, eneo la ekari 19 lililo mkoani Tanga na mahgari sita.

Katika akauti, TFF ina jumla ya Sh milioni 33.5 na Tenga amesema fedha hizo zimebaki kiasi hicho baada ya kufanya malipo ya mkutano mkuu Sh million 135, malipo ya maandalizi ya kikosi cha Tanzanite Sh milioni 33.5 na yote yamefanyika ndani ya wiki tatu.

Lakini kati ya Jumanne au Jumatano, malipo ya Sh milioni 664 kutoka TBL zitaingia ndani ya akaunti ya TFF na Juni mwakani, idadi kama hiyo ya fedha itaingia tena.

Katika makabidhiano, Malinzi alismhukuru sana Tenga na kusema ameonyesha juhudi kubwa nay eye anaahidi kuendelea kumuita rais hata kama muda wake umekwisha.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic