Mechi ya Azam na Mbeya City iliyochezwa Azam Complex
yenyewe imeingiza sh. 15,973,000 kwa watazamaji 4,857 na kila klabu imepata sh.
3,953,162.
Hiyo ni rekodi katika uwanja huo unaomilikiwa na Azam
FC, timu pekee yenye uwanja mzuri nchini.
Mechi hiyo ilimalizika kwa sare ya mabao 3-3 na Mbeya
City ikabaki katika nafasi ya tatu na Azam ya pili.
Yanga iliyoibuka na ushindi kwenye Uwanja wa Taifa,
moja kwa moja ikapanda hadi kwenye nafasi ya kwanza.
Mashabiki walijitokeza kwa wingi mno, hadi ikalazimika
polisi kuzuia wengine wasiingie.
0 COMMENTS:
Post a Comment