March 28, 2014





Baada ya kutopewa nafasi katika mchezo uliopita dhidi ya Simba, baadhi ya wachezaji wakongwe wa Coastal Union wametoweka kambini klabuni hapo bila taarifa wakati timu hiyo ikiwa katika maandalizi ya mchezo ujao dhidi ya Mtibwa Sugar.


Chanzo cha habari kutoka ndani ya timu hiyo kilisema kuwa, baadhi ya wachezaji hao wakongwe wa timu hiyo, wameondoka kambini hapo bila taarifa huku wakiwa mitaani kuendelea na mambo yao binafsi.

Chanzo hicho kilisema kuwa kambini hapo hapaeleweki kwa sasa na hii ni baada ya vijana wa timu hiyo kupewa nafasi katika mchezo uliopita, baada ya wakongwe wa timu hiyo kutopewa nafasi kufuatia kufanya vibaya katika mchezo wao dhidi ya Azam FC.

“Wachezaji wakongwe asilimia kubwa ni kwamba hawapo kambini kwa ajili ya maandalizi ya mchezo ujao, wameondoka bila taarifa na wakijua fika kwamba Jumapili (keshokutwa) tuna mechi dhidi ya Mtibwa,” kilisema chanzo.

Alipotafutwa Mkurugenzi wa Ufundi wa Coastal, Nassor Bin Slum alisema kitendo cha kuwapa nafasi vijana yalikuwa ni mapendekezo kutoka kwa mwalimu wao lakini kitendo chao cha kuondoka kambini si sahihi.

“Mapendekezo ya vijana kocha ndiye aliyeamua, kitendo cha kuondoka kambini ni kwamba wamedhihirisha kweli hawana nidhamu, walitakiwa kuwa kambini kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wao wa Jumapili, hakuna aliyewafukuza pale, wameamua kuondoka wenyewe tu,” alisema Bin Slum.

Alipopigiwa simu Boban alisema: “Mi nipo nyumbani nafanya mambo yangu.” Kisha akakata simu. Wakati upande wa Nyosso naye bila maelezo mengi, alisema:  “Nipo nyumbani tu.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic