March 28, 2014



 
NIYONZIMA (KULIA) AKIPAMBANA NA KIIZA MAZOEZINI
Kasi, uwezo anavyoonyesha kiungo mchezeshaji wa Yanga, Hassan Dilunga, vimemfanya Kocha Mkuu wa Yanga, Mholanzi Hans van Der Pluijm kutamka kuwa hamuhitaji Mnyarwanda Haruna Niyozima katika mechi zilizosalia za Ligi Kuu Bara.


Kocha huyo mwenye kitambi cha ‘kishkaji’, ameweka wazi msimamo wake huo mara baada ya Yanga kuifunga Tanzania Prisons mabao 5-0 juzi, ambapo amesema Dilunga ndiye anayemhitaji na siyo Niyonzima kwa kuwa kipindi hiki ni cha mapambano makuu.

Pluijm alisema kwamba anafurahi kuona kijana mdogo kama Dilunga anaonyesha uwezo mkubwa, ambapo anaamini ni kutokana na kipaji alichonacho pamoja na kuzingatia anachomfundisha.

Kuhusu Niyonzima, kocha huyo alisema: “Unajua hawa wachezaji wote wana vipaji na wote ni wazuri lakini kuna vitu ambavyo Dilunga anavyo vinavyonifanya nimwanzishe katika kikosi cha kwanza kwenye mechi za hivi karibuni na pengine zilizobakia.

“Timu inahitaji ushindi katika kila mchezo uliobaki ili tutwae ubingwa, kwa staili anayocheza Dilunga kutokana na mechi zilizobaki, anastahili kuanza kikosi cha kwanza, anapigana, anakaba na pia anachezesha timu kwa ustadi mkubwa zaidi.

“Angalia kombinesheni yake na (Frank) Domayo, ni viungo ambao wote wanacheza kwa kutegemeana, wote wanakaba pamoja na kuchezesha timu pamoja, nafikiri hiki pia ni kigezo kingine kizuri kwa Dilunga.”

Niyonzima alikuwa na uhakika kwenye kikosi cha kwanza kwa muda mrefu, lakini ujio wa Dilunga aliyesajiliwa akitokea Ruvu Shooting msimu huu, umesababisha Niyonzima anayesifika kwa uchezaji wa madoido kukosa namba.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic