March 28, 2014





Wakati Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) likisubiri taarifa kutoka serikalini kuhusu thamani ya kioo cha mlango kilichovunjwa na winga wa Simba, Ramadhan Singano ‘Messi’, Bodi ya Ligi imesema kuwa lazima Messi akumbane na rungu jingine kutoka kwao.


Bodi hiyo imesema kuwa inataka kutoa adhabu hiyo ili iwe kama fundisho kwa wengine kwani kilikuwa ni kitendo cha kudhamiria.

Messi alivunja kioo hicho Jumapili iliyopita baada ya timu yake kuchezea kichapo cha bao 1-0 mbele ya Coastal Union kwenye Uwanja wa Taifa, ambapo hasira za kufungwa akazihamishia kwenye mlango wa vyumba vya kubadilishia nguo kwa kuupiga teke.

Ofisa Mtendaji wa Bodi la Ligi, Silas Mwakibinga alisema licha ya mchezaji huyo kulipa fidia za kioo hicho, bodi watakaa kuangalia ni adhabu gani atatakiwa kupewa kama onyo.

“Lilikuwa tukio ambalo kila mmoja aliliona, siyo kusema ilikuwa bahati mbaya, hivyo baada ya mambo mengine kumalizika, suala lake haliwezi kuachwa hivihivi, kuna adhabu nyingine itatolewa kama fundisho kwa wote,” alisema Mwakibinga.

Tayari mchezaji huyo ameomba radhi kwa kitendo chake kwa kile alichosema zilikuwa ni hasira za kukosa mabao ya wazi, hususan dakika ya mwisho alipobaki na mlinda mlango wa Coastal.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic