Hofu imetanda kwenye kambi ya Yanga baada ya
benchi la ufundi la timu hiyo kufanya kikao kizito na wachezaji wao na
kuwalisha kiapo wakihofia hujuma kutoka kwa wapinzani wao, Simba.
Hatua hiyo imekuja siku chache kabla ya Yanga
kuivaa Simba katika Ligi Kuu Bara, keshokutwa Jumapili kwenye Uwanja wa Taifa
jijini Dar.
Yanga kwa sasa ipo Bagamoyo wakati Simba
imejichimbia Zanzibar, maalum kwa ajili ya mchezo huo.
Chanzo kutoka ndani ya wachezaji wa timu hiyo,
kilisema mara baada ya kurejea nchini wakitokea Botswana kuvaana na BDF,
walikutana na benchi nzima la ufundi na kuwasisitiza suala zima la rushwa.
Chanzo hicho kilisema, benchi hilo la ufundi
limeshtukia kuwepo na mchezo mchafu unaopangwa na wapinzani wao, hivyo
wamejipanga kuhakikisha wanakabiliana nayo.
“Kiukweli viongozi tayari wamemshtukia mbinu
chafu zote zinazofanywa na wapinzani wetu, wamejua njia zote walizopanga
kuzitumia.
“Tulikaa na viongozi na kila mmoja kula kiapo
kuwa hataisaliti timu katika mechi dhidi ya Simba, lengo kubwa tushinde mechi
hiyo ili tujiwekee mazingira mazuri ya ubingwa,” kilisema chanzo hicho.
Aidha , katika hatua nyingine, wachezaji
Deogratius Munishi, Juma Abdul, Edward Charles, Rajab Zahir, Pato Ngonyani, Hassani
Dilunga, Danny Mrwanda, Haruna Niyonzima, Mrisho Ngassa, Amissi Tambwe na Simon
Msuva walipewa adhabu ya kuzunguka uwanja na kocha mkuu wa timu hiyo, Hans van
Der Pluijm baada ya timu yao kufungwa mabao 2-1 mazoezini, juzi.
0 COMMENTS:
Post a Comment