Kocha wa Costa Rica, Paulo Wanchope amezichapa
kavukavu na mlinzi wa uwanjani huko Panama.
Wanchope ni mshambuliaji wa zamani wa Man City
pia Derby County za England.
Alizichapa baada ya kuzozana na mlinzi aliyekuwa
akizuia mmmoja wa vijana wasiingie eneo alilokuwa akilinda, lakini Wanchope
akafungua na kumuingiza.
Hali hiyo ilimfanya mlinzi huyo kupandwa na hasira na kuanza kumshambulia Wanchope ambaye alijibu mashambulizi.
Hata hivyo Shirikisho la Soka la Costa Rica
limekataa, katakata kulizungumzia suala hilo.
AKIWA MAN CITY. |
AKIWA DERBY COUNTY, HAPA ANAPAMBANA NA MARC VIVIEN FOE WAKATI WA UHAI WAKE AKIWA WEST HAM. |
GAZETI NALO HALIKUWA NYUMA, LIKAUNASA MCHEZO MZIMA... |
0 COMMENTS:
Post a Comment