|
HAWA MADOGO HATARI ASEE... |
Timu ya vijana ya Azam FC chini ya miaka 20 (U20)
iliwafanyaia mbaya Ndanda FC ya Mtwara inayoshiriki Ligi Kuu Bara baada ya
kuifumua mabao 3-2 katika mchezo wa kirafiki uliopigwa leo asubuhi kwenye
Uwanja wa Azam Complex, Chamazi jijini Dar es Salaam.
Vijana wa Azam wanaonekana kuimarika kutokana na soka la kasi
wanalocheza mwanzo mwisho.
Mchezo huo ulikuwa wa kasi na ushindani, huku vijana
hao wa Azam wakifanikiwa kuzima mashambulizi ya Ndanda iliyosheheni wachezaji
nyota akiwemo beki na nahodha wa timu hiyo, Paul Ngarema.
|
MCHEZAJI WA NDANDA AKIBURUDIKA NA GAZETI LA LEO LA CHAMPIONI. |
|
KOCHA IDDI CHECHE AKIMPA KIJANA MAELEKEZO. |
|
NDANDA WAKIPASHA... |
0 COMMENTS:
Post a Comment