Straika wa zamani wa Yanga, Said Bahanuzi na
aliyekuwa kipa wa Simba, Hussein SharifF ‘Casillas’, wote wamefanikiwa kusaini
mkataba wa mwaka mmoja kuichezea Mtibwa Sugar ya Turiani, Morogoro.
Bahanuzi msimu uliopita alikuwa akiitumikia
Polisi Moro kwa mkopo akitokea Yanga huku Casillas alikuwa nje ya uwanja kwa
muda mrefu akiwa na majeraha ya ugoko.
Casillas amesema amesaini mkataba maalum wa
mkopo na anaamini ataisaidia timu hiyo kupambana kwenye ligi. Bahanuzi alisema,
anashukuru kutua Mtibwa baada ya kuachwa na Yanga na kwani amepewa mkataba
rasmi wa mwaka mmoja.
“Nimejiunga na Mtibwa kwa mkataba wa mwaka
mmoja baada ya kuachana na Yanga, naamini ushirikiano nitakaoupata huku
tutaiwezesha timu yetu kufanya vizuri msimu ujao,” alisema Bahanuzi.
0 COMMENTS:
Post a Comment