Simba SC, leo inacheza mechi ya kirafiki dhidi
ya SC Villa ya Uganda kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam lakini kocha wake,
Dylan Kerr amesema kikosi chake kipo vizuri na kitashinda mechi hiyo kutokana
na rekodi yao.
Kerr ameliambia Championi Jumamosi kuwa, akiwa
kambini Zanzibar wachezaji wake walionyesha uwezo mkubwa kiasi cha kuweza
kufunga mabao 17 katika mechi tano ambazo huchukua dakika 450 huku ikifungwa
mabao matatu tu.
Simba iliifuga Polisi ya Zanzibar mabao 4-0
kisha ikashinda mabao 4-0 dhidi ya Jang’ombe Boys, mabao 2-1 dhidi ya Kombaini
ya Zanzibar pia ikaifunga KMKM mabao 3-2 na ikaifunga Black Sailor mabao 4-0.
“Unaiona hiyo rekodi? Tupo vizuri kwani wakati
naichukua timu ilikuwa na matatizo kadhaa na sasa mambo yamebadilika na kila
mchezaji ana hamu ya kupata ushindi.
“Mashabiki wajue kitu kimoja, sikuandaa kikosi
changu kwa ajili ya mechi hii tu, bali na mechi nyingine ambazo tutakutana nazo
katika ligi na matokeo tuliyoanza nayo Zanzibar nataka yaendelee katika mechi
zote.”
Kerr raia wa Uingereza alisema sasa timu yake
inacheza soka la kasi huku wakitumia pasi fupifupi kuelekea lango la adui na
kila mchezaji anapata nafasi ya kucheza.soka.
0 COMMENTS:
Post a Comment