Kiungo ‘rasta’, Thabani Kamusoko yupo katika
hatua za kusaini mkataba wa kuichezea Yanga akitokea FC Platinum ya Zimbabwe,
amewaambia mashabiki wa timu hiyo kuwa amekuja kufanya kazi na siyo masihara.
Kamusoko raia wa Zimbabwe jana Ijumaa alifanya
mazoezi kwa mara ya kwanza na Yanga kwenye Uwanja wa Karume, Dar es Salaam
chini ya uangalizi wa Kocha Hans van Der Pluijm na Katibu Mkuu, Dk Jonas
Tiboroha.
Katika mazoezi hayo, Kamusoko alionekana kufanya vizuri katika
mazoezi ya kukaba na kupiga mipira mirefu kwa washambuliaji na mashuti makali
kuelekea lango la adui.
Kamusoko alisema: “Naijua vizuri Yanga tangu
mwaka 2002, ni timu nzuri yenye wachezaji wenye ushindani, nitapambana
kuhakikisha napata nafasi ya kucheza.
“Nimekuja Tanzania kufanya kazi, nataka
mashabiki wajue hivyo na wasidhani nimekuja kufanya mambo mengine hapa, nipo
kazini.”alisema Kamusoko’’.
0 COMMENTS:
Post a Comment