SIMBA ILIYOANZA LEO, KERR AKABADILI WACHEZAJI SABA KATIKA KIPINDI CHA PILI. |
Simba imeibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya URA ya Uganda ambayo
imekuwa ikiwafunga kila inapocheza nao.
Simba imeibuka na ushindi wa mabao hayo ikiwa
na wachezaji baada ya Peter Mwalyanzi kuumia huku Kocha Dylan Kerr akiwa amemaliza
sub zote, hivyo Simba ikaendelea kupambana ikiwa na wachezaji 10 uwanjani.
Mara zaidi ya tatu, Simba imekuwa ikilala
kutoka kwa URA kwa misimu minne sasa.
Hivyo ushindi wa leo, Simba ilikuwa imemaliza
uteja kutoka kwa wakusanya mapato hao wa Uganda.
Mashujaa wa Simba leo ni Mganda Juuko Murshid
na Mrundi, Kelvin Ndayisenga waliofunga mabao hayo mawili wakati Simba ikiamka katika
kipindi cha pili baada ya kuonekana imelala katika kipindi cha kwanza.
0 COMMENTS:
Post a Comment