Ili kujiandaa vizuri kuhakikisha
inaishinda Nigeria mwezi ujao, Taifa Stars itacheza mechi ya kirafiki dhidi ya
Oman.
Taifa stars itasafiri hadi Muscat, Oman
kucheza mechi ya kirafiki dhidi ya Oman.
Gazeti la Oman la Oman Newspaper
limeripoti kocha wa Oman akionyesha kufurahishwa na mechi mbili za kirafiki.
Kocha huyo amesema mechi yake ya kwanza
itakuwa Agosti 24 dhidi ya Tanzania kabla ya kuivaa Yemen Agosti 28.
Juhudi za kuwapata watu wa TFF
kuthibitisha zilikuwa ngumu, lakini taarifa nyingine za ndani zimethibitisha.
“Kweli nimesikia timu wakati inakwenda
Uturuki itaanzia Oman kwanza kwa ajili ya mechi hiyo ya kirafiki.
“Baada ya hapo itaendelea na safari kwenda
Uturuki ambako itaweka kambi. Lakini bado sijapata uhakika wa hilo,” kilieleza
chanzo.
0 COMMENTS:
Post a Comment