June 9, 2017



Mbio za usajili zinaendelea kwa nguvu kubwa, gumzo ni klabu tatu, Simba, Yanga na Singida United, sasa kuhusu kiungo wa Simba, Jonas Mkude kuna habari inayomhusu na ametamka yeye mwenyewe.

Mkude ambaye mara kadhaa amewahi kuhusishwa kuwaniwa na Yanga, ameamua kuweka wazi kuwa atatua ndani ya kikosi cha Yanga kwa ajili ya kukitumikia msimu ujao kwa kutoa sharti moja kubwa ambalo ni klabu hiyo kumpatia shilingi milioni 70.

Mkude kwa sasa yuko huru kujiunga na timu yoyote baada ya mkataba wake na Simba kudaiwa kumalizika hivi karibuni, ikiwa ni mwisho wa mkataba wake wa shilingi milioni 60 aliosaini kuitumikia Simba miaka miwili iliyopita.

Kiungo huyo amesema atakuwa tayari kusaini mkataba na Klabu ya Yanga kwa dau la kuanzia milioni 70 kwenda juu kutokana na kiwango alichonacho kwa sasa.

“Kwa upande wangu nipo tayari kutua Yanga kwa dau la kuanzia milioni 70 na kuendelea hadi shilingi milioni 150 na siwezi kusaini chini ya hapo, nipo tayari kutua katika timu yoyote kwa kiasi ambacho tutakubaliana kwa kuwa kiwango changu kipo vizuri.

“Lolote linaweza kutokea kuanzia sasa, tusubiri kila kitu kitakuwa wazi muda si mrefu na wadau watajua nitasaini wapi kwa ajili ya msimu ujao, wasiwe na hofu.


“Mimi ninachoangalia ni maslahi popote pale watakaofanikiwa kunipa dau ambalo tutakubaliana, nitakuwa tayari kufanya kazi,” alisema Mkude.

SOURCE: CHAMPIONI

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic