August 20, 2018


Staa wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ ameifungukia ishu ya kufilisiwa na benki inayosemekana inamdai baada ya kukopa na kushindwa kulipa. Nay aliliambia Ijumaa Wikienda kuwa, siyo kweli kwani mali zake zote zipo na hajawahi kuwa na mkopo kwenye benki yoyote.

Ishu ya Nay kufilisiwa ilianza kusambaa mitandaoni baada ya mashabiki kudai msanii huyo kwa sasa hana jipya kwani benki hiyo walik-wenda nyumbani kwake na kutaifisha mali zake zote zikiwemo nyumba na magari anayomiliki baada yakushindwa kulipa deni. Nay alisema hakuna ishu kama hiyo na hakuna mali yake yoyote iliyopigwa mnada kwa sababu mali zake zote zipo na hafikirii kwenda kukopa sehemu yoyote.

“Ni stori tu ambazo watu wameamua kuzungumza na watu kuzungumza siyo dhambi kwa sababu mimi ni staa, kwa hiyo watu wakiwa wanaongea vitu kama hivyo huwa sishtuki, nawaa-ngalia tu,” alisema Nay.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic