September 1, 2020

 


TARIQ Seif, kiungo mshambuliaji wa zamani wa Klabu ya Yanga amesaini dili la miaka miwili ndani ya Klabu ya Polisi Tanzania. 


Seif alipokuwa akikipiga Yanga alipewa jezi namba 10 ambayo kwa sasa amekabidhiwa mshambuliaji mpya Yacouba Sogne raia wa Burkina Faso.


Polis Tanzania imezidi kujiimarisha kwa ajili ya msimu mpya wa 2020/21 ambapo imesajili nyota wengi wenye uzoefu ikiwa ni pamoja  na Daruesh Saliboko aliyekuwa ndani ya Lipuli.


Dirisha la usajili ambalo lilifunguliwa Agosti Mosi limefungwa Agosti 31.

10 COMMENTS:

  1. hivi huyu si ni yule jamaa utopolo walikuwa wanajisifu kuwa wamesajili mchezaji toka Misiri...allipokelewa kwa maneno ya shangwe

    mfano ya wanaopokelew uwanja wa ndege

    ReplyDelete
    Replies
    1. Ngoja tuone na usajili wenu wa wachezaji wazee mikia. Mnasajili mchezaji wa miaka 50. Hii mmevunja record. Hizi dalili za buncruptcy. Mtapata taabu sana kuwanunulia mechi.

      Delete
  2. Wazee wa visingizio. Hata mkifungwa 7 bado mtatafuta visingizio. Hiyo mnayemwita mzee alimweka mfukoni Samatta kwenye AFCON tena Samatta aliyechukua tuzo ya uchezaji bora wa ndani Africa na sio wachezaji wenu hao wa kuokoteza. Inferiority complex inawasumbua. Mmeshindwa uwanjani mmkekalia kashfa na visingizio.

    ReplyDelete
  3. mmesikia utopolo mwaka huu hakuna timu nne..walidhani Libya haitapata nafasi kwa sababu ya machafuko

    ombeni Libya washindwe kuthibitisha!
    Na siku nyingine mkipata chance sio kwenda kujiondoa wenyewe kwa kujifunga halafu kila siku wimbo wa UD Songo...wakati wenyewe mmeboronga kwa kujifunga na kujitoa

    ReplyDelete
  4. Unaongea kama mwehu unaiponda nchi yako mwenyewe?

    ReplyDelete
    Replies
    1. Timu nne Tanzania ili wale ambao hawajatolea jasho ubingwa waende kimataifa na Yanga waanze kushangilia timu za wageni kama ilivyokuwa mwaka jana na juzi?tunajua Tuisila na mwenzake ni zawaidi toka kwa AS Vita kwa fadhila ambazo Yanga iliifanyia AS Vita ilipokuja cheza na Simba.
      Tunatambua ugumu Simba iliyopitia hadi kufikia robo fainali kitu ambacho kilisababisha Tanzania kuongezewa timu toka mbili yaani mshindi wa ubingwa na wa shirikisho.Walikuwa wakicheza Congo na Misiri huku nyumbani Yanga wanashangilia saana..Wacongo na Wamisiri wakija hapa wakifungwa wenzetu wanasononeka..Jitihada za Simba zika zaa matunda yaliyonufaisha nchi..Simba ikaanza vibaya kwa UD Songo. Tukarudi kule kwenye vifijo na nderemo Simba ilipokuwa ikifungwa 5-0.Isingekuwa Faida ya Timu nne Yanga asingecheza na Zesco.

      Delete
  5. Kati ya yanga na simba nani alitolewa mapema caf cl last season?

    ReplyDelete
  6. Hao vichwa vyao vitupu. Fujo hadi kuwachania mashati wapenda amani jambo ambalo kwengine lingevunja amani na TFF isilifungie msco itoe kama ilivo Fanya wahuni wengine hivi karibuni. Mpira hauleti chuki lakini kujuwana, kupendana na kufurahishans. Hao hata Okwi na Kagere walisema ni wazee na sasa Onyango aliemnyima furaha Samata

    ReplyDelete
  7. sawa Simba alitolewa mapema na Yanga WAKAJITOA hatua iliyofuata..wala hawakuenda hatua mbili zaidi ya Simba.

    Suala ni namna timu ilivyotolewa.Baada ya sare ya Dar timu ya Zesco ilihitaji ushindi Zambia na Abdul Aziz Makame wa Yanga aliifungia timu ya Zesco bao la pili. Zesco ikasonga mbele kwa 2-1. Simba iliondolewa na UD Songo kwa UD Songo kupata faida ya goli la ugenini..Nadhani utatambua nani aliondolew kishujaa.
    Pia tujikumbushe katika hiyo season Yanga alikuwa ametwaa kombe la ubingwa au la shirikisho la Tanzania?
    Msimu uliopita Simba ilicheza hadi robo fainali jambo ambalo liliiongezea point Tanzania hivyo ikapewa timu nne

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic