Na Saleh Ally
TOKEA enzi za kocha Alex Ferguson,
Manchester United ilionyesha kuvutiwa kwa kiasi kikubwa na kazi ya kiungo wa
Athletic Bilbao ya Hispania. Juhudi zao za kumnasa pamoja na kwamba walitoa dau
zuri, zikakwama.
Manchester United ilitoa dau la pauni
milioni 24 (zaidi ya Sh bilioni 67) kumnasa Ander Herrera Aguera, lakini bado
Bilbao wakakataa kumuachia. Haikuishia hapo, United iliendelea kumfuatilia kwa
juhudi kubwa hadi ilipomnasa msimu huu kwa dau la pauni milioni 29.
Huenda wengi walishangazwa na juhudi
hizo za Manchester United kutaka kumnasa kiungo huyo mwenye umri wa miaka 24
sasa. Ana nini, labda sababu ni ipi?
Mwisho wamefanikiwa kumpata na
imegundulika Barcelona pia ilikuwa ikifanya juhudi za chinichini kumnasa
Herrera lakini kiungo huyo alikuwa na ndoto siku moja aichezee Real Madrid.
Tayari yuko Manchester United na
katika mechi chache tu alizocheza za kirafiki akiwa chini ya Louis van Gaal
huko Marekani, kiungo huyo ameonyesha kweli anastahili kuitumikia timu hiyo.
Swali, anaweza kuwa suluhisho la
matatizo ya kiungo? Uwezo mkubwa alionao Herrera kucheza kama kiungo wa ulinzi
au kiungo mgawaji, mchezeshaji kweli unaweza kumaliza tatizo kubwa la kiungo
lililoonekana msimu uliopita?
Van Gaal ana nafasi ya kuchagua
anataka amchezeshe sehemu ipi, lakini ameonyesha ana uwezo mkubwa wa kukaba na
kilichoelezwa kuwa uchezaji wake ni staili ya Kiingereza badala ya Kihispania
kweli kimeonekana.
Kwa muda mfupi amejichanganya na
wachezaji wa Manchester na kuonekana kama amekuwa nao kwa muda mrefu. Kizuri
zaidi, hata wachezaji wengine wa United wameonyesha kumkubali, ni dalili njema
kwamba watataka kumsaidia ili awe msaada kwenye timu.
Ujio wake unaweza kuwa raha kwa
wengine na chachu kwa baadhi kama Marouane Fellaini ambaye huenda atalazimika
kuondoka kwa kuwa hakuwa na msimu mzuri tangu alipotua United akitokea Everton.
Takwimu zinaonyesha anaweza kuwa dawa
mpya ya matatizo ya Manchester United kwenye safu ya kiungo ingawa wapo wenye
hofu kwamba kuna viungo walitoka kwenye timu zao wakionekana ni msaada,
wakafeli baada ya kutua United.
Takwimu zinaonyesha katika maisha yake
ya soka la kulipwa kuanzia akiwa Zaragoza B, msimu wa 2008-09, Herrera amecheza
jumla ya mechi 229, amefunga mabao 19 tu.
Ingawa ameshaonyesha ana uwezo wa
kufunga, lakini United inamtaka kwa ajili ya uunganishaji wa timu, hivyo
haiwezi kuwa na hofu na suala la ufungaji kwa kuwa wenye uwezo wa kufanya hivyo
inao wengi.
Mechi 186 za La Liga akiwa amefunga
mabao 15, zinaonyesha ana uzoefu wa kutosha na hatakwenda kufundishwa nini cha
kufanya.
Msimu uliopita alimaliza La Liga akiwa
na wastani wa pasi 47, alitengeneza nafasi 53 safi za kusaidia kufunga lakini
tano ndiyo zikazaa mabao. Tatizo lake kubwa ni faulo, msimu huo wa 2013-14 alifanya
faulo 46 lakini akalambwa kadi 7 tu za njano.
Tatizo jingine alilonalo ni kwamba,
kama mchezo ‘ukichafuka’, watu wakaanza kucheza kibabe, yeye huwa hautulizi,
badala yake anauchafua zaidi, kiaina unaweza kusema ni mbabe.
Uwezo wake umefanya wachambuzi wengi
kumuweka kwenye daraja la wachezaji nyota kwenye kiungo kama Andres Iniesta
(Barcelona), Mesut Ozil (Arsenal) na Cesc Fabregas (Barca/sasa Chelsea).
Angalia takwimu za msimu uliopita za Herrera,
Ozil, Fabregas na Iniesta.
PASI ASILIMIA PASI ZA
MABAO MABAO MECHI DAKIKA
Ferrera 47
80.6%
5
5
33
2,548
Iniesta
63
90.7%
7
3
35 2,488
Fabregas
60
87%
13
8
36 2,463
Ozil 63
88%
9
5
26 2,149
FIN.
0 COMMENTS:
Post a Comment