July 30, 2014



Straika nyota wa TP Mazembe ya DR Congo na timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Mbwana Samatta, amesema kinachoifanya Stars isifanye vizuri, suala la wachezaji wengi kung'ang'ania kucheza nyumbani, linachangia.


Samatta anaamini kama wengi wakikubali changamoto na kuamua kucheza nje ya Tanzania, itakuwa msaada kwa Taifa Stars.

Nyota huyo wa zamani wa Simba, sasa anakipiga TP Mazembe, ndiye mchezaji tegemeo sambamba na mwenzake Thomas Ulimwengu.

Hivi karibuni Stars iliambulia sare ya mabao 2-2 kwenye mchezo wa kutafuta tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika dhidi ya Msumbiji, matokeo ambayo siyo mazuri kwa timu hiyo ambayo Jumapili itacheza mchezo wa marudiano nchini Msumbiji.

Samatta amesema kuwa ili Stars iweze kufanya vizuri, ni lazima wachezaji ambao wanakipiga kwenye timu za hapa nchini na kupata mafanikio, waende kutafuta timu nyingine nje ya nchi ili kuongeza viwango vyao ambavyo vitakuja kuisaidia Stars.

“Naweza kusema tunashindwa kufanya vizuri kwa sababu wachezaji wetu wengi wanang`anga`nia kucheza soka la nyumbani na wala hawajitumi kutafuta nafasi za kucheza soka la kulipwa nje ya nchi, hivyo ni lazima mastaa wote wakatafute nafasi kwenye soka la kulipwa ili tuweze kupata maprofesheno wengi wa kuisaidia Stars,” alisema Samatta.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic