YAMETIMIA, DI MARIA HUYU HAPA NDANI YA MANCHESTER Hatimaye Angel Di Maria ametua na kusaini mkataba wa miaka mitano kuichezea Manchester United. Mkataba huo ndiyo rekodi mpya ya usajili baada ya Man United kukubali kutoa pauni milioni 59.7 ambazo ni pauni milioni 60 ili kumpata. Atakuwa akilamba mshahara wa pauni 200,000 kwa wiki, anachukua nafasi ya pili kwa mshahara mkubwa baada ya nahodha wake, Wayne Rooney.
0 COMMENTS:
Post a Comment