January 28, 2015


Kiungo mkongwe wa Simba anayeichezea Azam FC kwa mkopo, Amri Kiemba, amesema kuwa kwa sasa yupo tayari kuanza mazungumzo na timu yoyote inayomhitaji hata ikiwa Yanga.

Kiemba yupo Azam kwa mkopo na mpaka msimu huu utakapomalizika, atakuwa amebakiza miezi sita.


Kiemba amefunguka kuwa, soka ndiyo kazi yake, hivyo anaweza kutua timu yoyote kama ataelewana nao hata kama ikiwa Yanga ambao ni mahasimu wa Simba, yupo tayari kwenda kuitumikia.

“Sijajua nitakwenda wapi baada ya kumalizana na Simba na nikishatoka kwa mkopo hapa Azam mwisho wa msimu, timu yoyote naweza kuzungumza nayo kuanzia sasa kwa ajili ya kujua msimu ukiisha nakwenda wapi.


“Mpira ni kazi yangu, kwa hiyo siwezi kuchagua timu kwa kuwa mpira ni uleule, cha msingi ni juhudi, hata kama Yanga watakuja nitazungumza nao, kama tutakaa chini na kuelewana hakutakuwa na tatizo,” alisema Kiemba.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic