Kiungo mkongwe wa Simba anayeichezea Azam FC kwa
mkopo, Amri Kiemba, amesema kuwa kwa sasa yupo tayari kuanza mazungumzo na timu
yoyote inayomhitaji hata ikiwa Yanga.
Kiemba yupo Azam kwa mkopo na mpaka msimu huu
utakapomalizika, atakuwa amebakiza miezi sita.
Kiemba amefunguka kuwa, soka ndiyo kazi yake,
hivyo anaweza kutua timu yoyote kama ataelewana nao hata kama ikiwa Yanga ambao
ni mahasimu wa Simba, yupo tayari kwenda kuitumikia.
“Sijajua nitakwenda wapi baada ya kumalizana
na Simba na nikishatoka kwa mkopo hapa Azam mwisho wa msimu, timu yoyote naweza
kuzungumza nayo kuanzia sasa kwa ajili ya kujua msimu ukiisha nakwenda wapi.
“Mpira ni kazi yangu, kwa hiyo siwezi kuchagua
timu kwa kuwa mpira ni uleule, cha msingi ni juhudi, hata kama Yanga watakuja
nitazungumza nao, kama tutakaa chini na kuelewana hakutakuwa na tatizo,” alisema
Kiemba.
0 COMMENTS:
Post a Comment