Kocha Mkuu wa Simba, Goran Kopunovic, amesema kuumia kwa mchezaji
wake, Emmanuel Okwi, katika mchezo wa timu hiyo dhidi ya Azam kuliwachanganya.
Katika mchezo huo, Okwi alitolewa uwanjani hapo akiwa hajitambui
baada ya kugongwa kichwani na beki wa Azam FC, Aggrey Morris, wakiwa katika harakati
za kugombania mpira ambapo mchezo
huo ulimalizika kwa timu zote kufungana bao 1-1.
Akizungumza jijini Dar Kopunovic amesema kuumia kwa
mchezaji huyo, kulimfanya yeye pamoja na benchi lake la ufundi kushindwa
kufikiria mchezo huo na badala yake kuwaza mchezaji huyo anaendeleaje.
“Nilikuwa na hofu baada ya kuumia kwa Okwi kwa sababu kwanza ni
mchezaji nyota ndani ya kikosi chetu, lakini pia ukirudi katika hali ya
ubinadamu, afya ya mtu ni muhimu sana kuliko jambo lolote lile.
“Yaani sikuwa katika hali ya kawaida katika dakika kama ishirini
za mwisho ambapo hata mchezo wenyewe sikuwa nafuatilia kwa umakini, muda wote
nilikuwa nawaza kuhusu afya ya mchezaji wangu,” alisema Kopunovic.
0 COMMENTS:
Post a Comment