Kocha Zdravko Logarusic
amekumbana na kipigo chake cha kwanza tokea aliporejea nchini Kenya.
Loga aliyewahi kuinoa
Simba, sasa anainoa AFC Leopard ambayo ameiongoza katika mechi nne za ligi ya
nchi hiyo akishinda mbili, sare moja na sasa kipigo kimoja.
Mechi yake ya kwanza
alikwenda suluhu dhidi ya Chemelil, halafu akazishinda Nairobi City 1-0 na
Nakuru All Stars 3-1 kabla ya kukutana na kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa Ulinzi
inayomilikiwa na Jeshi la Kenya.
Loga pia amewahi kuinoa Gor
Mahia ambao ni wapinzani wakubwa wa AFC Leopars anayoinoa sasa.
0 COMMENTS:
Post a Comment