'ABRAMOVICH' AKIMPONGEZA HANS VAN DER PLUIJM MARA BAADA YA KUWASILI JIJINI DAR ES SALAAM |
Mabingwa wa Tanzania, Yanga wamewasili jijini Dar es Salaam, leo
na kupokelewa Kiongozi wa Wazee wa Yanga, Ibrahim Akilimali maarufu kama
Abramovich.
Akilimali alikuwa kwenye Uwanja wa Ndege wa
Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), kuwapokea wachezaji, makocha na viongozi wa
Yanga waliowasili wakiyokea nchini Tunisia.
Yanga ilikuwa nchini Tunisia kupambana na
Etoile du Sahel ambayo iliitoa Yanga kwa kuifunga bao 1-0 na kusonga kwa jumla
ya mabao 2-1 baada ya sare ya 1-1 jijini Dar.
Abramovich alichofanya ni kumpongeza Kocha
Mkuu, Hans van der Pluijm, benchi la ufundi pamoja na wachezaji kwa kazi nzuri.
“Mmecheza vizuri sana, mmeonyesha soka la
uhakika. Mmetolewa lakini kila mmoja kaona juhudi zake,” alisema Akilimali.
Wachezaji na makocha wa Yanga waliwasili na
kuingia kwenye gari kwenda makao makuu ya klabu hiyo katika makutano ya
Jangwani na Twiga ambako walipokelewa kwa furaha na wanachama.
Yanga imeng’olewa lakini ilionyesha soka
safi na la ushindani na kuwapa Waarabu hao wa Tunisia wakati mgumu wakiwa kwao.
Karibuni nyumbani,yaliyopita si ndwele tugange yajayo.
ReplyDeleteMmefanya vizuri ila bahati haikuwa yenu,na ndio maana wale mabingwa wa kuzomea hawakujipanga barabarani kuzomea,"AU sijui kwa kuwa wanabembeleza ili muwafunge AZAM"