Rais wa Tanzania, Jakaya
Kikwete amewashauri Yanga kujiandaa zaidi kwa ajili ya michuano ya kimataifa
msimu ujao.
Rais Kikwete alikutana na
wachezaji wa Yanga Dubai wakitokea Tunisia wakati yeye akiwa njiani kwenda
Marekani.
Kikwete alipata nafasi ya
kuzungumza na wachezaji hao, wengine wakapiga naye picha.
Pia aliwasifia kwa mchezo
mzuri huku akisisitiza wanapaswa kujituma zaidi na kujiandaa vilivyo ili msimu
ujao wafanye vizuri zaidi.
Yanga ilifungwa bao 1-0 na
Etoile du Sahel ya Tunisia, hivyo kung’olewa katika michuano ya Kombe la
Shirikisho kwa jumla ya mabao 2-1.
Kwa ujumla Yanga wako vizuri kuanzia wachezaji,makocha,viongozi na kifedha pia.
ReplyDeleteUshauri wasibadilishe kikosi ila wakiboreshe kwa maandalizi mapema.