Uongozi
wa klabu ya Yanga, leo umemtambulisha kiungo wake mpya, Deus Kaseke.
Kaseke
ametua Yanga akitokea Mbeya City baada ya kusaini mkataba wa miaka miwili kwa
dau la Sh milioni 35, jana.
Kaseke
ametambulishwa mbele ya waandishi wa habari katika makao makuu ya klabu hiyo
naye kusema amefurahia kujiunga na Yanga.
“Ninahitaji
mafanikio, Yanga ni sehemu sahihi, nafurahi kuwa hapa. Ninaahidi kujituma zaidi
ili niweze kufanya vizuri nikiwa na Yanga,” alisema.
0 COMMENTS:
Post a Comment