November 27, 2015


Beki wa pembeni wa Simba, Hassani Kessy, amefunguka na kutaja sababu inayomzuia asiongeze mkataba ni timu hiyo kutoshiriki michuano ya kimataifa Afrika.


Kufikia mwezi ujao, Kessy atakuwa amebakiza miezi sita katika mkataba wake na kwa mujibu wa kanuni za Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa), anaruhusiwa kufanya mazungumzo na klabu nyingine inayomhitaji ikiwemo Yanga ambayo inatajwa kumuwania kwa ukaribu.

Yanga itashiriki katika Ligi ya Mabingwa Afrika kutokana na kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara msimu uliopita.

Kessy amesema mipango aliyojiwekea ni kucheza soka la kimataifa nje ya Tanzania na ndiyo maana amekuwa akisita kusaini mkataba mpya Simba.

“Sifikirii kuongeza mkataba wa kubaki kuendelea kuichezea Simba katika kipindi kingine, licha ya viongozi kuhitaji huduma yangu.

“Ninaamini kama nikipata timu inayoshiriki michuano ya kimataifa, basi bila kuchelewa nitasaini mkataba ili iwe rahisi kwaku kutimiza ndoto zangu kwa kuwa nitaonekana kimataifa,” alisema Kessy.


3 COMMENTS:

  1. Sidhani kama mawazo yake ni sahihi, kessy bado ni kijana mdogo ambaye anahitaji kushauriwa kwa karibu.
    Kwa nafasi anayopata Simba alitakiwa aitumie na kuipa Simba ubingwa ili waweze kushiriki hayo mashindano ya kimataifa akiwa katika timu ya kwanza ya Simba "first eleven"
    Kwa timu zilizokwisha jiimarisha kama Azam Fc na Yanga Sc Hassan Kessy hana nafasi hata kidogo mbele ya wachezaji wenye uzoefu na uwezo mkubwa kama Shomari Kapombe na Juma Abdul.
    Ajifunze kwa Ramadhan Singano, alikuwa lulu Simba , na alikwisha jihakikishia namba katika kikosi cha kwanza, leo hana namba Azam Fc wala hana nafasi tena ya kuitwa timu ya taifa, inaumiza sana, vilabu viaache kuwadanganya wachezaji wadogo na kuwapoteza kabisa katika ramani ya soka kwa ahadi ya fedha za muda mfupi.
    Kessy tulia Simba ucheze mpira, ama nenda kakae benchi TP Mazembe, lakini sio benchi la Azam au Yanga.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic