August 24, 2017




Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), linaomba radhi wanafamilia wote wa mpira wa miguu kutokana na makosa ya maandishi yaliyoonekana kwenye utambulisho wa Ngao ya Jamii iliyotolewa Jumatano Agosti 23, 2017.

Ngao hiyo ilitolewa mara baada ya mchezo uliokutanisha timu za Simba SC na Yanga SC za Dar es Salaam kwenye Uwanja Mkuu wa Taifa jijini. Katika mchezo huo, Simba ilishinda kwa mikwaju ya penalti 5-4 dhidi ya Yanga na kutwaa Ngao hiyo. 



Katika Ngao ya Jamii, kulikuwa na neno Community Sheild badala ya Community Shield, jambo lililozua mjadala mkubwa miongoni mwa wapenda soka nchini.

Watanzania hususani wanafamilia ya mpira wa miguu popote pale, TFF hatujapokea vizuri mwonekana wenye makosa kwenye Ngao hiyo ya Jamii kama ambavyo wadau hawajapokea vema suala hili.

Kutokana na makosa hayo, Kaimu Katibu Mkuu wa TFF, tayari amechukua hatua za kinidhamu kwa watumishi waliohusika kadhalika kuwasiliana na uongozi wa Simba SC kuirejesha Ngao hiyo ili kufanyiwa marekebisho yatakayobaki kwenye kumbukumbu sahihi.


Hatutegemei tukio kama hili kujirudia tena.

1 COMMENTS:

  1. Pia tunataka maneno ya kiingereza yasitumike yatumike ya kiswahili yaani ngao ya jamii. Tunataka marekebisho hayo ya kutumia kiswahili yaanze kuonekana kwenye hiyo ngao kwa msimu wa 2018-2019.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic