March 26, 2014



Mabingwa wa soka Tanzania, Yanga leo wameonyesha bado wana nguvu ya kuwania kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara baada ya kuwachapa Prisons ya Mbeya kwa mabao 5-0.

Katika mechi hiyo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, Yanga walionyesha hawana mchezo baada ya mabao kalamu hiyo ya mabao kuonyesha wamejirekebisha kutokana na kale kamtindo ka kupoteza nafasi.
Yanga ilipata bao lake la kwanza kupitia mshambuliaji nyota Emmanuel Okwi aliyefunga kwa mkwaju wa adhabu. Baadaye Okwi aliumia na nafasi yake ikachukuliwa na Hamisi Kiiza.
Kiiza alifunga mabao mawili, mengine mawili yakafungwa na mshambuliaji mwenye kasi, Mrisho Ngassa na nahodha Nadir Ali Haroub ‘Cannavaro’ ambaye siku hiyo amecharuka katika upachikaji mabao.
Maana yake Yanga imefikisha pointi 46 na inaendelea kubaki katika nafasi ya pili nyuma ya vinara Azam FC.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic